Vituo vipo vingi lakini sisi tulienda kigogo na tulikuta vitu mbalimbali vilivyoletwa na watu au mashirika mbalimbali.Tuliwapelekea
ndoo,mabeseni,dawa za meno,mafuta,sabuni,nguo,godoro,maji ya
kunywa,juice na biscuit kwa watoto,malapa na vyandarua.Ila tukaja
kugundua wanawake wengi wana uhitaji wa taulo za kike(pads) na nguo za
ndani.Kwa hiyo wengine mtakaofatia kupeleka misaada mnaweza kuangalia na
eneo hilo mnalisaidia vipi. Tulikuta watu wengi wanafua nguo zao baada ya kuletewa maji yale ya kwenye magari.
Pia chakula cha mchana kilikuwa kinapikwa japo wanalalamika wakati
mwingine watu kama wazee kukosa chakula maana hawana nguvu za kupanga
foleni.Na pia wazamiaji wanasababisha wale walengwa kukosa chakula.
Doreen na mtoto
Ruben na mtoto Sabrina ambae anaumwa kifua sababu ya kulowana na mvua na maji ile juzi,pembeni ni Khadija Mwanamboka.
Mtoto huyu ana miezi miwizi mama yake wakati wa kujinusuru ilibiri ambebe kwenye pochi kubwa ili kumnusuru.
Mh.Iddi
Azan mbunge wa Kinondoni alikuwa akitupa maelezo kuhusu swala la vyoo
lilivyokuwa na changamoto kwa vituo vingine kasoro hapo.Maana shuleni
hapo kuna vyoo angalau pamoja na vyoo vya msaada vile ya mobile.
Baada ya kukabidhi msaada tukaanza kuzungukia kuona nyumba zilivyoathiriwa na mvua na mafuriko.
0 comments:
Post a Comment