JAFO AAGIZA MANISPAA DODOMA IPIME HARAKA VIWANJA NA AMFAGILIA MBUNGE MAVUNDE KWA KUWAJALI WANANCHI



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akizungumza na wananchi kata ya Iyumbu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akisaini kitabu cha wageni katika shule ya msingi Iyumbu.

Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza na wananchi katika kata ya Iyumbu.

Mbunge wa Viti maalum Felista Bura akizungumza na wananchi wa kata ya Iyumbu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akifurahi jambo na Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akisalimia na baadhi ya viongozi wa kata ya Iyumbu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akiwapungia mkono wananchi wa Iyumbu.

baadhi ya waannchi kwenye mkutano Iyumbu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akipokea zawadi


……………


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi kuhakikisha wanapima viwanja haraka ili kuufanya mji wa Dodoma uendane na kasi ya ongezeko la idadi ya watu wanaohamia Dodoma na kuufanya mji uliopangwa kwa utaratibu unaoeleweka.


Jafo ameyasema hayo leo katika hafla fupi ya kuweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Shule ya Sekondari Iyumbu-Dodoma Mjini,ambapo pia ametumia nafasi hiyo kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwatumikia na kuwaletea maendeleo wananchi wake na kuahidi kuendelea kumpa ushirikiano katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wake wa Jimbo la Dodoma Mjini.


Mbali na hilo, Jafo ameagiza fedha kiasi cha sh.milioni 10 zilizopo kwenye akaunti ya kata hiyo ambazo zilitakiwa kutumika kupaulia darasa la shule ya sekondari Iyumbu kutumika kujenga madarasa manne.


Kwa upande wake, Mavunde amesema katika Manispaa ya Dodoma kuna upungufu wa vyumba vya kusomea zaidi ya 1000.Amesema wamekubalina na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kuanzisha kampeni maalumu ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa kupitia wadau mbalimbali ambapo wao watapokea vifaa tu kama Saruji.


Awali katika hafla hiyo,Mkurugenzi wa Manispaa Kunambi amesema tayari Manispaa imeshatoa Sh.Milioni 10 kusaidia ujenzi huo na pia ameahidi kusimamia ujenzi wa Sekondari hiyo ili kuwaondolea adha wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata shule za Sekondari.


Wakizungumzia hatua hiyo, Wananchi wa kata Iyumbu wameshukuru sana jitahada za viongozi katika kuwaletea maendeleo na kutatua changamoto zao na kuahidi kujitolea kukamilisha ujenzi huo.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments: