Waandishi wa habari watakiwa kuwa makini na habari za uchaguzi 2015 wanazoziripoti


Mhandisi Kisaka kutoka TCRA makao makuu akitoa somo kwa viongozi wa vyombo vya habari kanda ya Nyanda za juu kusini.

Na Edwin Moshi, Mbeya
Vyombo vya habari nchini vimetakiwa kuwa makini na kuripoti habari za uchaguzi mkuu wa mwaka huu kufuata maadili na weledi wa taaluma hiyo ili kufanikisha uchaguzi huo kwa amani

Hayo yamesemwa leo jijini Mbeya na Mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA wakati wakiwapa semina mameneja na wamiliki wa vyombo vya habari vilivyopo kanda ya nyanda za juu kusini semina iliyofanyika jijini Mbeya

Akizungumza katika semina hiyo wakati wa hotuba ya kufungua semina hiyo Naibu Mkurugenzi idara ya utangazaji TCRA makao makuu Bw. Fredrick Ntobi amewasisitiza waandishi wa habari kote nchini kuhakikisha wanafuata maadili ya kazi zao ili kuepuka madhara yatakayoweza kujitokeza pindi watakapotoa taarifa potofu kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka huu na chaguzi nyingine zitakazofuata baada ya uchaguzi huo

"Naomba muwe makini na uandishi wenu wa habari maana ninyi ninyi ndio mtakaofikishwa mahakamani, ninyi ndio mtakaofikishwa The Heag, ajirini watu wenye professional (taaluma) ya habari, hii itasaidia kuepuka kauli za uchochezi, zitawamaliza na niwahakikishie sisi kama mamlaka tupo makini na tutafuatilia vyombo vyote vya habari" amesema Ntobi

Kwa upande wake Mhandisi mkuu idara ya Utangazaji TCRA makao makuu Mhandisi Andrew Kisaka amewataka washiriki kuhakikisha wanazingatia usawa katika kutoa taarifa za uchaguzi na kuepuka upendeleo wa baadhi ya vyama

"Unakuta CHADEMA mnawapa dakia mbili kujieleza halafu CUF mnawapa dakika 20 hili sio sawa, hakikisha mnatoa kipindi kilichowapa fursa sawa wagombea wote bila upendeleo

Aidha Kisaka amewaonya waandishi wa habari kuacha kujiingiza kwenye siasa kwa kushabikia wagombea fulani na kuingiza itikadi zao katika kuripoti habari za uchaguzi kwa kuwa itasababisha kuwagawa wananchi na kuona kituo chako kina upendeleo jambo ambalo halitakiwi

Katika semina hiyo washiriki wamepewa nafasi ya kuuliza ma swali na kutoa ushauri wa masuala mbalimbali yaliyowasilishwa kwa lengo la kurahisisha utekelezaji wa mambo hayo katika vyombo vyao vya habari wanavyofanyia kazi
 Semina ikiendelea
 Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada katika semina hiyo
 Waandishi wa habari wakiandika vitu muhimu
Mwandishi wa habari akichangia mada katika semina hiyo.
Share on Google Plus

About Gadiola Emanuel

0 comments: