KAMISHNA WA SHERIA NA UENDESHAJI WA MAGEREZA, DKT. JUMA MALEWA ATEMBELEA GEREZA LA MAHABUSU MORIGORO

  Muonekano wa nje wa Gereza la Mahabusu Morogoro ambapo gereza hilo linauwezo wa kuhifadhi Wafungwa na Mahabusu 144
  Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akitia saini kwenye Kitabu cha Wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Gereza la Mahabusu Morogoro baada ya kuwasili Gerezani hapo tayari kwa ziara ya kikazi akikiwa ameongoza na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro na Maafisa Waandamizi wa Magereza kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Dar es Salaaam.
  Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza(wa pili toka kulia) akikagua maeneo mbalimbali ndani ya Gereza la Mahabusu Morogoro katika ziara yake ya kikazi aliyoifanya Novemba 1, 2013(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro, Naibu Kamishna wa Magereza, James Selestine(kushoto) ni Mthibiti Mkuu wa Fedha wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Gideon Nkana.
Baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Magereza wa Gereza la Mahabusu Morogoro wakiwa timamu kwa kazi za siku hiyo wakati Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(hayupo pichani) alipotembelea Gerezani hapo.Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza
Share on Google Plus

About Gadiola Emanuel

0 comments: